Translate

Friday, June 15, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA 12)

Katika sehemu iliyopita tumeona Athumani akijinunulia magazeti,na kukutana na jalada la warembeo,hatimae kufanikiwa kumwona Rehna,ambae ndie mpenzi wake .Kama kawaida yake Athumani,aliweza kumpigia simu Rehna ,na kupanga waonane Bamaga mchana,lakini mkewe Athumani,ambae ni jini,alikuwa akiwasikiliza maongezi yao kwa makini,baada ya hapo Asha alienda kwa njia ya upepo,mpaka chumbani kwa Rehna,alipofika akamkaba Rehna mpaka akaanza kutapika,Asha alifanya hivyo,Lakini Rehna hakuwa akimwona Asha. (sasa endelea.....) Athumani akaendesha gari mpaka kwenye ufukwe wa bahari,akaiona hoteli nzuri maeneo ya Coco beach.Akaongea na mhudumu wa hoteli,na kuchukuwa chumba namba 23,Wakiwa chumbani wamejipunzisha kitandani,Athumani na Rehna,wakiwa wanashikana sehemu za mwili,Asha akaingia chumbani na kuvua nguo zake,akajitupa kitandani.Athumani akaushika uume wake kuingiza kwa Rehna,Lakini Asha akaudhika na kuingiza yeye mahala pake,kisha Asha akachukuwa mkono wake na kuuingiza sehemu ya Rehna,Ilikuwa ni mbinu ya khali ya juu,aliyotumia jini Asha.Kwa mkono wa Asha aliweza kuukunja na kuupekecha mpaka Rehna akawa anasikia maumivu makali badala ya starehe.Rehna akamwambia Athumani ,mbona unaniumiza? Athumani akamjibu Rehna vumilia baby,mbona mimi najisikia raha kama nikiwa na mke wangu.(nini kitatokea?angalia sehemu ijayo)

Tuesday, June 12, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA KUMI NA MOJA)

Katika sehemu ya kumi tumeona jinsi alivyopata msukosuko wa moyo,baada ya kushuhudia tukio,ambalo ,bado anajiuliza mpaka leo,hivi yule nilyemuona amekumbatiwa na jamaa,alikuwa mke wangu?jibu hajalipata,ila endelea sehemu hii,utapata ukweli wa mambo.(sasa endelea.....) Mwandishi wa kujitegemea Thomas,alifanikiwa kutoa jalada maalumu,katika gazeti la warembo,kwa ajili ya kumzungumzia Rehna.Ilikuwa majira ya saa mbili asubuhi,gazeti la warembo lilikwisha sambaa mitaani.Athumani kwa muda huo,alikuwa akielekea kazini,akiwa njiani,aliweza kujinunulia magazeti 2,uhuru na mzalendo,katika kupitisha macho kwenye meza ya magazeti,akaona picha kubwa ya binti,anakuja kwenye hisia,kama kuna sehemu,alikwisha muona.Akachukuwa nakala moja,akaangalia kwa makini na kusoma,akaona maelezo yako sahii,ni kweli anamfaham binti yule,Rehna.Akajinunulia nakala moja inayomzungumzia Rehna,na kupanda gari,kulekea kazini.Athumani alipofika kazini,akachukuwa simu yake ,na kumpigia Rehna.Wakasalimiana na kukumbushana siku waliyokuwa pamoja coco beach. Athumani akampongeza Rehna,hongera nimeona umetoka kwenye gazeti la warembo.Rehna akamjibu Athumani,sina taarifa yeyote juu ya jalada la warembo.Athumani akamwambia Rehna,usijali ninalo,nitakupa baadae.naomba tuonane Bamaga majira ya mchana.Rehna akamjibu sawa dear. Asha mke wa Athumani alikuwa ni jini,ambae hakutaka mumewe Athumani ajuwe kwamba yeye ni jini.watu wengi wamekuwa wakiishi na majini,pasipo kuelewa.hii imesababisha mifarakano mingi katika ndoa.Wakati Athumani akiongea na Rehna,Asha ambae ndie mke wa Athumani,alikuwa palepale ofisini,akimsikiliza mumewe.Asha akatafakari nini afanye,akaondoka mpaka nyumbani kwa Rehna.Alipofika akaingia kama upepo,mpaka chumbani kwa Rehna,Asha akamkaba Rehna shingoni,mpaka Rehna akajisikia uchungu kama anakufa,akamuachia.Rehna akaanza kutapika,mfululizo,Asha alikuwa amesimam anacheka,kumbuka Asha ndie anamuona Rehnna.(nini kitatokea?endelea sehemu ifuatayo

NAMPENDA KUTOKA MOYONI-(SEHEMU YA KUMI)

Katika sehemu ya tisa.tumeona Thomas,akikutana na Mrembo Rehna,Baada ya ktambulishana,akachukuwa maelezo ya Rehna na picha,kwa ajili ya kwenda kutoa kwenye gazeti la warembo.pia tumeona Athumani akienda kituoni kwa ajili ya kupata taarifa za kesi na siku ya kwenda kuhudhuria mahakamani,baada ya hapo,athumani alirejea nyumbani kwake,lakin hakuweza kumkuta mke wake.akampigia simu,lakini ilikuwa haipatikani,mwisho akaondoka na gari kuelekea mjini.Aliendesha gari taratibu,huku akiangaza huku na kule,akamwona mke wake amekaa pembeni mwa hoteli na jamaa mnene ,akiwa amemkumbatia mkewe.(sasa endelea....) Athumani akasogeza gari mpaka pale karibu na mkewe na jamaa walipokaa.Athumani akashuka kwenye gari akiwa na hasira nyingi,alipokaribia akaona kibibi kizee,kinalia.palepale alipokaa mkewe na jamaa yake,akaangaza macho pande zote nne,hakuweza kumwona mke wake ,wala yule jamaa.Athumani akashangaa sana,yule bibi akamuliza Athumani ,una matatizo gani mjukuu wangu?Athumani akamjibu,kuna jamaa alikuwa na mwanamke wamekaa hapo ulipo kaa,nashangaa nimeshuka kwenye gari siwaoni,nakuona wewe.Bibi akamjibu Athumani,sikiliza mjukuu wangu,hapa mimi nipo tokea jana kwenye kiti hichi,hakuna mtu mwengine aliyekaa hapa.Athumani akafikiria sana,mara simu ikawa inalia,kuangalia namba ,akaiona simu ya mke wake Asha,Hakuweza kuamini akapokea simu,Atumani akamuliza mke wake,uko wapi?Asha akamjibu mimi nipo nyumbani.Athumani akamuiza tena Asha,mbona nilikuja sijakuona?Asha akamjibu,nilikuwa nyumba ya pili,nilienda kusuka.Athumani akawasha gari na kuelekea nyumbani kwake,Alipofika akamkuta mkewe.Athumani alikuwa na hasira lakini ,hakuwa na ushaidi kamili wa tukio la mkewe.Asha akamtayarishia chakula,baada ya hapo,wakawa wanakula chakula pamoja.Athumani alimpenda kutoka moyoni Asha,lakini bado ,hajatambua kwamba Asha ni jini.Mengi ya kusisimua tutayaona baadae.wakati ,Athumani akiwa anajaribu kumsaliti, Asha na wapenzi wengine.

Monday, June 11, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI( SEHEMU YA TISA)

Katika sehemu iliyopita tumeona Polisi baada,ya kupewa taarifa za wizi,waliweza kufanikiwa kuwakamata wahalifu wote,waliohusika kwenye uvamizi wa nyumba ya Athumani.Waliweza kufikishwa kituoni,kwa ajili ya kufungua jalada la kesi,ili kuipeleka kesi mahakamani.(sasa endelea......) Ilikuwa ni siku ya jumanne asubuhi,Thomas ambae alikuwa ni mwandishi wa habari wa kujitegemea,alikuwa katika pita zake mitaani,akakutana na msichana mrembo,aliyejulikana kwa jina la Rehna.Wakati Thomas alipokutana na Rehna,ilikuwa nje kidogo ya nyumbani kwao.Thomas akamsalimia Rehna,hujambo dada?Rehna akamjibu sijamba Kaka.Thomas akajitambulisha kwa Rehna kama ifutavyo,Samahani dada,Naitwa Thomas,ni mwandishi wa habari wa kujitegemea.Rehna akamjibu,nashkuru kwa kunifahamisha,naitwa Rehna,ni mwanafunzi. Thomas akamwambia Rehna,napenda nipate maelezo yako kwa ujumla,pamoja na picha nitakupiga,wewe ndio mrembo utakaonekana kwenye gazeti la warembo.Rehna akatoa maelezo yote na kumpatia Thomas.baada ya maelezo,Thomas akampiga picha 4.Alipomaliza akachukuwa namba ya simu,wakaagana. Athumani aliondoka,nyumbani kwake kwa ajili ya kuelekea kazini.Alipofika kazini akaendela na kazi mpaka majira ya saa 7 mchana.Baada ya hapo,akaelekea kituoni,kwa ajili ya kujuwa siku ya kesi.Alipofika kituoni,akakutana na Afisa mpelelezi na kupewa maelezo kamili.Athumani alitakiwa kuhudhuria kesi mahakamani tarehe 12 julai. Athumani akaondoka kuelekea nyumbani.Alipofika nyumbani kwake,akamkuta mke wake,hayupo. Athumani akampigia simu mkewe,lakini simu ya mkewe ilikuwa haipatikani.Athumani akatoka nyumbani na kuendesha gari mpaka mjini.Alikuwa akiendesha gari,huku akitupa macho yake pande zote mbili.Ghafla akamuona mkewe amekaa kwenye kiti pembeni mwa hoteli,akiwa amekumbatiana na Jamaa mmoja mnene.(nini kitatokea?angalia sehemu ya kumi)

Sunday, June 10, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA NANE)

Katika sehemu iliyopita tumeona tukio lililotokea nyumbani kwa Athumani,baada ya kundi la watu wasiojulikana kuvamia hapo nyumbani kwa Athumani,na kupora vitu mbalimbali,baada ya tukio,Athumani na mkewe Asha,wakaondoka kuelekea mjini,na kuripoti kituo cha polisi,kisha sehemu anayofanyia kazi,baada ya hapo,wakaelekea baharini kwa ajili ya kujipunzisha.Wakiwa huko,Athumani alimuliza mkewe,kama ana upo wowote,kuhusu tukio zima kwa ujumla,kisha wakapata wazo,huwenda rafiki yake Asha,akawa chanzo cha tukio.Wakaondoka kuelekea kituo cha polisi kuripoti,Polisi wakaamua kwenda nao mpaka nyumbani kwa chiku.Walipofika wakaizingira nyumba,na kutoa tangazo maalum.(sasa endelea.....) Polisi waliamuru kila mtu aliye katika nyumba ile,atoke kwa usalama wake,kabla jeshi la polisi ,halijachukuwa mkondo wake wa sheria.Watu wakaanza kutoka mmoja baada ya mwengine,kulikuwa na watu 12,ndani ya nyumba ile,wengine 3,walikuwa wapangaji katika nyumba ile.Kati ya hao,wale wote waliokuja kupora nyumbani kwa Athumani.Baada ya wote kutoka,polisi akamuliza Athumani,je unawafahamu hawa?Athumani akajibu,hawa sita ndio waliokuja kupora asubuhi ya leo,nyumbani kwangu.Polisi wakawatia pingu wale wote sita,pamoja na chiku.Kisha polisi akawauliza wale waporaji,vitu viko wapi? mmoja wao akajibu,vipo ndani chumbani kwa chiku. Polisi na Athumani,wakaelekea ndani ya chumba cha chiku,waliweza kukuta vitu vingi,pamoja na silaha za kila aina,ndani ya chumba.Wakatoa vitu vyote na kuvipakia kwenye gari,kisha wakaelekea kituoni.Walipofika kituoni wakfungua kesi zidi ya waporaji,na kuandaa jalada,kwa ajili ya kuipeleka kesi mahakamani. Athumani akamwambia mkewe Asha,umeona faida ya mashoka kama hawa?Asha akamjibu mumewe,yaani sikutegemea,kweli kikulacho.....ni kinguoni mwako.Kwa hili mume wangu nimejifunza mengi sana.

Saturday, June 9, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA SABA)

Katika sehemu iliyopita tumeona nyumbani kwa Athumani,kundi la watu wasiojulikana,lilivamia na kupora vitu mbalimbali,lakini hapakuwa na majeruhi yeyote karika tukio hilo.Baada ya tukio,Athumani na mkewe Asha wakaondoka kuelekea mjini.(sasa endelea.....) Athumani aliendesha gari taratibu mpaka mjini,akaenda kwa tajiri yake kutoa taarifa,baada ya hapo,Athumani na mkewe Asha,wakaelekea kituo cha polisi,kwa ajili ya kutoa taarifa, kamili ya tukio lililotokea nyumbani kwao.kisha baada ya hapo wakaelekea ufukweni mwa bahari kwa ajili ya kupunguza mawazo.Athumani alikuwa akifikiria jumapili alipokuwa na Rehna,wakati Asha alikuwa mwenye furaha,kwa sababu,ni kipindi kirefu,alikuwa hajawahi kufika maeneo ya ufukwe wa bahari. Majira ya saa 9,mchana ,Athumani akamuliza mke wake,unafikiri ni sababu gani,tumepata tukio kama hili?Asha akamjibu mumewe,kwa kweli mpaka muda huu,nimekuwa nafikiri,na kuwaza lakini jibu bado sijalipata.Athumani akamuliza tena Asha,unae rafiki wa karibu,anaekuja nyumbani kukutembelea?Asha akamjibu mumewe,ninae rafiki mmoja,lakini anakaa mbali kidogo. Athumani akamwambia Asha,tuondoke mara moja.Wakapanda kwenye gari na kuondoka.Athumani akaenda mpaka kituo cha polisi,wakatoa taarifa ya huyo msichana.polisi 4,wakaondoka nao,na kuelekea nyumbani kwa msichana huyo,aliyejulikana kwa jina la chiku.Walipofika nyumbani kwa chiku,polisi wakaizunguka nyumba yote,wakatoa tangazo maalumu.(nini kitatokea?endelea sehemu ya nane)

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA SITA)

Katika sehemu iliyopita tumeona Rehna na Athumani wakiwa Coco beach,kwa ajili ya kujipunzisha kwa muda,kisha baadae ,majira ya saa 7 ,mchana waliondoka kuelekea nyumbani,Athumani alimfikisha Rehna nyumbani kwao,kisha akaelekea nyumbani kwake,alipofika nyumbani,mke wake Asha,akafungua geti la nyumba,kisha Athumani akaingiza gari ndani,Baada ya hapo,wakakaa sebuleni na kula chakula pamoja.(sasa endelea.....) Ilikuwa ni siku ya jumatatu asubuhi,majira ya saa 2,kikundi cha watu wasiojulikana walivamia nyumbani kwa Athumani,na kupora vitu vingi vya thamani,lakini hakuna madhara ya kumjerui mtu yeyote hapo nyumbani kwake,Athumani na mkewe Asha,waliomba usalama wa roho zao,bila kujali hasara ya vitu watakavyochukuwa.Baada ya dakika 20,kundi hilo likatoweka na mali na kukimbilia mji mwengine,kwa mwendo wa haraka.Athumani alimwambia mkewe,usihudhunike,pesa ni makaratasi,hasara ni roho.Asha alikuwa na mawazo mengi ya tukio kama hilo,lakini hakuweza kupata majibu ya haraka.Alifikiria mambo mengi sana,na kujaribu kufikiri,nini chanzo cha tukio,lakini mawazo yote,hayakuweza kumpa majibu.Athumani akamwambia mkewe ajitayarishe,wapate kutoka pamoja,kwa sababu,haitakuwa jambo jema kubaki peke yake,kwa tukio ambalo limetokea.Asha akaingia chumbani kutafuta nguo,atakayoweza kuipata,ili aweze kuvaa. Baada ya muda kidogo,wakaondoka hapo nyumbani,kuelekea mjini.

Friday, June 8, 2012

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA TANO)

NAMPENDA KUTOKA MOYONI :SEHEMU YA TANO Katika sehemu iliyopita tumeona Athumani,akiwa anatumiana ujumbe mfupi na Rehna ,na kukubaliana kukutana Bamaga siku ya pili.(sasa endelea...) Athumani alikuwa anaendesha gari lake taratibu,akiwa anaelekea Bamaga.Rehna aliondoka nyumbani kwao mapema,baada ya kuaga anaenda kanisani.Athumani alifika Bamaga na kumkuta Rehna akiwa amekwishafika anamsubiri.baada ya kukutana uso kwa uso,wakapeana mikono na kukumbatiana.Athumani akamwambia Rehna ,ingia kwenye gari,tukatembee Baharini.Rehna akaingia kwenye gari,na wakaelekea Baharini.walienda mpaka COCO BEACH.Athumani akaegesha gari lake pembeni,na wakaanza kutembea ufukweni mwa bahari,wakiwa wameshikana mikono.Waliendelea na starehe zao ,mpaka majira ya saa saba mchana.ndipo walipoamua kuondoka baharini.Athumani akawasha gari moto,na kumpeleka Rehna mpaka karibu na nyumbani kwao.Athumani alipomfikisha Rehna kwao,akaondoka kuelekea nyumbani kwake.Asha alikuwa anatayarisha chakula cha mchana,mara akasikia sauti ya gari la mumewe,akaenda kufungua mlango wa geti,Athumani akaingiza gari mpaka ndani.Asha akamwambia mumewe,nilikuwa nikupigie simu,lakini kabla sijafanya hivyo ukatokea.Athumani akamjibu mkewe,samahani kwa kuchelewa,mazungumzo yalikuwa marefu kidogo.Asha akaweka chakula sebuleni,wote kwa pamoja wakaanza kula chakula cha mchana.Kwa upande mwengine Rehna alikuwa amechanganyikiwa sana na Athumani.alikuwa na anatamani kuwa na Athumani muda mrefu zaidi.(nini kitatokea?sasa endelea sehemu ya sita

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA NNE)

Katika sehemu iliyopita tumeona Athumani akiagana na Thomas,baada ya chakula,kisha Athumani kurejea nyumbani kwake na kukutana na mke wake Asha,Baada ya kusalimina Asha akaenda bafuni kumpelekea maji ya kuoga.Wakati mumewe akiwa anaoga,Asha alikwenda kuweka chakula sebuleni.Athumani alipomaliza kuoga,akaenda sebuleni kula chakula na mke wake.Walipomaliza kula chakula,wakaenda chumbani kujipunzisha.Baada ya muda ,Asha alikuwa amelala usingizi.(sasa endelea.....) Baada ya Athumani kupata ujumbe kutoka kwa Rehna,alifurahi sana,kuona kwamba upo uwezekano mkubwa wa kumpata Rehna.Akavuta pumzi na kunza kuandika ujumbe kwa Rehna.Sikiliza Rehna,mimi nimekupenda kutoka moyoni,naomba kesho jumapili tuonane.kisha akautuma kwa Rehna.Baada ya kupokea ujumbe huo,Rehna akaujibu,kama ifuatavyo,baby usiwe na wasiwasi,nifuate Bamaga ,saa nne asubuhi.kisha akautuma kwa Athumani.Baada ya kupata ujumbe huo,Athumani akamjibu Rehna kama ifuatavyo,usiwe na khofu,nitafika muda huo.kisha akamwambia nakutakia usiku mwema.tutaonana kesho.kisha akamtuia Rehna.Ujumbe ulimfikia Rehna akiwa na usingizi mwingi,baada ya kusoma ujumbe,akamjibu .Ahsante dear wangu usiku mwema.Rehna akalala usingizi,Asubuhi na mapema,Asha akaamka na kutayarisha maji ya kuoga.Athumani a kaenda bafuni kuoga,Wakati huo ,Asha alikuwa anatayarisha chai ya asubuhi.Baada ya kumaliza kuoga na kuvaa nguo,Athumani akaenda sebuleni kunywa chai.Baada ya kunywa chai,ilikuwa majira ya saa tatu na nusu,Athumani akamuaga mke wake,naenda mjini mara moja,kuna mtu naenda kufanya nae mazungumzo.Asha akamjibu mumewe,sawa ila usichelewe mume wangu.Athumani akamjibu,sitochele9wa mke wangu.Athumani akawasha gari moto,na kuelekea Bamaga.(nini kitatokea?endelea sehemu ya tano)

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA TATU)

Katika sehemu iliyopita tumeona Athumani na rafiki yake Thomas.Alikuwa Thomas ndio aliyemkaribisha Athumani nyumbani kwake,kwa ajili ya chakula cha mchana.Baada ya Thomas ,kumtambulisha Athumani kwa mke wake na binti zake wawili,Athumani alivitiwa sana na binti wake rehna ,kwa sababu alikuwa na mvuto wa kupendeza.(sasa endelea......) Athumani akaingiza gari ndani,na kufunga mlango mkubwa.Kama kawaida yake Asha akamkumbatia mumewe na kumpa busu la nguvu.Baada ya hapo ,Asha akaenda bafuni na kumpelekea maji,kwa ajili ya mumewe kuoga.Alipomaliza kuweka maji bafuni,akaenda chumbani,na kumwambia Mumewe ,aende bafuni kuoga.Athumani akachukuwa taulo,na kuelekea bafuni kuoga.Wakati huo ,Asha alichukuwa chakula na kupeleka sebuleni,kwa ajii ya mumewe kupata chakula cha jioni.Athumani alipomaliza kuoga na akaenda sebuleni ,kupata chakula na mkewe.Baada ya chakula wakaenda chumbani kujipunzisha.Thomas alikuwa nyumbani kwake na familia yake.Athumani alijitupa kitandani na mke wake Asha.Baada ya muda Asha akawa amelala hoi.Athumani akatuma ujumbe mfupi kwa Rehna.hujambo mtoto mzuri?Rehna alipopata ujumbe kutoka kwa Athumani ,akamjibu ,na kumwambia,sijambo dear wangu.Athumani baada ya kuona majibu ya haraka kwa Rehna,Athumani akatuma ujumbe mwengine kwa Rehna,sikiliza baby,nimetokea kukupenda sana ,wewe ni mrembo,mzuri wa kuvutia,naomba unikubalie penzi langu kwako,nami nitakuwa mwenye furaha,na upendo wa dhati kwako.kisha akautuma ujumbe huo kwa Rehna.Ujumbe ulipomfikia Rehna,akausoma kwa makini sana.kisha akaujibu kama ifuatavyo,sikiliza dear wangu,hata mimi nimekupenda sana,ila naomba uwe kweli na usinidanganye ,nitakupa penzi la kweli.(nini

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA PILI)

Katika sehemu ya kwanza tumeona Asha na Athumani wakiwa shuleni,hadi kufika wakati wakawa na uamuzi wa kuishi kama mke na mume,baada ya kufunga ndoa,na kuanza maisha yao DaresSalaam.Athumani alikuwa Afisa masoko wizarani.Maisha yao ,yalikuwa mazuri sana.(sasa endelea.....) Thomas ni katibu mkuu ,wizara ya viwanda na biashara,alikuwa ni rafiki mkubwa wa Athumani,Thomas alikuwa ni mtu mwenye msaada mkubwa kwa Athumani,na ndiye aliyefanya mipango ya kazi kwa Athumani.Siku moja Thomas ,alimualika nyumbani kwake Athumani,kwa ajili ya chakula cha mchana.Athumani alifika kwa Thomas muda muwafaka,Thomas akaanza kumtambulisha Athumani kwa mke wake Irene,baada ya hapo ,akawaita watoto wake wawili,ambao wote ni mabinti,Maria na Rehna.Athumani alipowaangalia wale mabinti,alivutiwa sana na Rehna kwa uzuri,aliokuwa nao.Rehna alikuwa na miaka 19,mwenye umbo la kuchanganya mwanaume yeyote duniani.Thomas akamkaribisha chakula Athumani,na wakaanza kula chakula.Baada ya chakula,thomas alikwenda chumbani kuongea na mke wake,muda huo Rehna alikuwa yupo na Athumani,Bila kuchelewa Athumani akamwambia Rehna chukuwa namba yangu ya simu,nitakuwa na maongezi na wewe.Rehna akachukuwa namba ya simu ,na akampatia namba yake.Thomas akatoka nje,na wakaagana na Athumani.Baada ya kuagana Athumani,akawasha gari moto na kuelekea nyumbani kwake.Alipofika akamkuta mkewe Asha ,ndio anamalizia kupika chakula.(nini kitatokea?sasa endelea sehemu ya tatu)

NAMPENDA KUTOKA MOYONI(SEHEMU YA KWANZA)

Katika maisha yangu ,tokea nikiwa mdogo,wakati nikiwa kijijini kwetu mwera,nilitokea kuwa rafiki mkubwa wa Athumani,wakati huo ,nilikuwa na miaka 7,na Athumani alikuwa na miaka 12,Katika familia yetu ya mzee jabiri,tumezaliwa 2,mimi asha,na aziza wa mwisho.Athumani na mimi ,tulibahatika kusoma shule moja ya msingi mwera,lakini ,Athumani alimaliza kwanza na kuendelea na sekondari ya Galanose iliyoko mjini Tanga.Miaka 4 ,baadae nami nikamaliza shule ya msingi na kuchaguliwa kwenda shule ya wasichana korogwe.Mahusiano yetu ,yalikuwa yakiendelea,kadri siku zilivyokuwa zikienda mbele.baada ya kuhitimu chuo kikuu,Athumani alipata kazi wizara ya viwanda na biashara,na alikuwa akifanya kazi Dare-sSalaam.Nilifanikiwa kumaliza kidato cha sita ,na sikubahatika kwenda chuo.Ndipo Athumani alipoamua kufunga ndoa na mimi.Miaka miwili baadae,tukafunga ndoa na kuanza maisha mapya ya ndoa mjini Dare-sSalaam.Kama mnavyoelewa maisha ya mjini yana misukosuko mingi na mambo mengi.Athumani alikuwa akifanya kazi kama afisa masoko wizarani,kazi ambayo ilikuwa na maslahi makubwa zaidi.Aliweza kubadilika kimaisha na kujenga nyumba nzuri maeneo ya Gongo la mboto,na pia alikuwa na usafiri wake mwenyewe.Kwa ujumla maisha ya Asha na Athuman,kama mke na mume,yalikuwa mazuri sana.Majirani zao,pia walikuwa wanajuwa upendo waliokuwa nao Asha na Athuman.(nini kitatokea?endelea sehemu ya pili