Translate

Monday, February 11, 2013

RAHA YA MAPENZI NI KUPENDWA(3)

Ilikuwa ni siku ya jumanne ,asubuhi na mapema,katika jiji la mwanza ambalo limezungukwa na milima ya aina mbalimbali kama mawe,alimasi na dhahabu.Wingu la kiza na kibari kwa mbali vilitatawla asubuhi ya jumanne.Ilikuwa saa 2 asubuhi,Hamisi alipowasha gari lake na kuelekea mjini.Alipokuwa njiani,gari lake lipata matatizo,baada ya tairi kupasuka katika mpira wa ndani.Hamisi akampigia fundi wa mjini ili waje kumsaidia.Kama tulivyoangalia sehemu iliyopita,tuliona Bakari ndio mpenzi wake Salma.Lakini hatukuweza kufaham Bakari kazi aliokuwa akifanya pale mjini mwanza.Hamisi akampigia fundi anaemuamini kabisa ,ambae ndie Bakari.Kwa wakati huo alikuwa amelala na Salma nyumbani kwake.Simu ilikuwa inaita lakini,Bakari alikuwa usingizini,Salma alikuwa macho pale kitandani,akaishika simu kwa wivu wake kuangalia nani anampigia mpenzi wake mpendwa.Salma akapata mshituko baada ya kuona namba ya Hamisi.Mara Bakari akashtuka usingizini na kumwambia Salma,nipatie simu.Salama akampatia simu Bakari,wakati simu ilikuwa inaita.Bakari akapokea simu na kuongea na Hamisi.Baada ya maongezi Bakari akamgeukia Salma na kumwambia,kuna kazi ya dharura inabidi niende kuifanya haraka,kama utapenda twende wote. Salma alikwisha fahamu mambo yanavyokwenda na aliyepiga alikwishamtambua ni Hamisi. Mpaka hapo utaona jinsi gani mapenzi,yalivyokuwa na mzunguko kati ya Bakari na Salma,pamoja na Hamisi na Salma.vilevile utaona kwa upande mwengine,utaona Mwanaidi amekuwa na mpenzi wake Hamisi kwa zaidi ya miaka kumi.Hapo utaona ni hatari sana kwenye mapenzi.na Huyu mfanyabiashara Hamisi ndio anae hudumia mzunguko wote.

No comments: