Translate

Monday, February 11, 2013

RAHA YA MAPENZI NI KUPENDWA(SEHEMU YA 2)

Hamisi akalipa pesa za nguo na vipodozi,waondoka kuelekea mjini,Walipofika mjini,wakaingia kwenye hoteli na kuagiza chakula.Baada ya kula chakula ,Hamisi akamchukuwa Salma na kumrudisha nyumbani kwao.Alipofika Salama akaagana na Hamisi.Baada ya hapo salma akaingia ndani kwao.Mama yake salma ,alikuwa akiitwa chausiku,akamkuta ukumbini,na kuanza kusalimiana na mama yake.Salma akaenda moja kwa moja chumbani kwake . Hamisi alitokea kumenda sana Salma,ndio maana alifanya jitihada zote,ili aweze kuwa na Salma.Kwa upande wa Salma kulikuwa ni tofauti sana.Salma alikuwa na mpenzi wake Bakari,alikuwa anampenda sana Bakari.Salma akaoga haraka na kuelekea kwa mpenzi wake Bakari. Baada ya kujiandaa na kuvaa mavazi ya gharama ambayo ,alinunuliwa na mpenzi wake Hamisi.Salma alikuwa amependeza sana.Akaagana na mama yake na kuondoka kuelekea kwa mpenzi wake wa moyoni. Bakari alikuwa chumbani kwake amejipunzisha,kutokana na uchovu wa kazi za kutwa nzima. Salma alipofika nyumba anakoishi Bakari akaenda moja kwa moja na kugonga mlango wa Bakari. Bakari akamkaribisha na wakaenda kitandani kujipunzisha.Salma alikuwa anampenda sana Bakari kupita Bakari anavyompenda Salma. Kwa wakati huo Hamisi alikuwa yupo nyumbani kwake amejipunzisha na mpenzi wake Mwanaidi.Hamisi na Mwanaidi wamekuwa wapenzi kwa zaidi ya miaka kumi.Kuna mengi mafunzo utayapata katika hadithi hii,kuhusiana na vituko na mambo yanayojitokeza kwa wapenzi duniani kote.
<

No comments: