Translate

Saturday, April 7, 2012

PENZI LA MASHAKA (SEHEMU YA KUMI NA MOJA)

Katika sehemu iliyopita tumeona ,Anita na Saimon,wakipanga mikakati ya kufungua kiwanda cha juice,na jinsi ya kuendesha biashara yao,Baada ya kuweka mikakati yao.Wakaagana na kurudi nyumbani.Alipofika nyumbani Sinza akakutana na rafiki yake peter.Baada ya kusalimiana,Peter akamwambia Saimon,nimekuja muda kidogo,ila mama yako,aliniambia umetoka na hautachelewa kurudi.(sasa endelea....) Saimon alikuwa amechoka sana,Akamwambia peter,najisikia nimechoka sana,sitaweza kutoka muda huu,labda tungefanya kesho asubuhi.Peter akamjibu saimon,usiwe na wasiwasi punzika,tutaeta kesho.Peter akamuaga Saimon na kuelekea nyumbani kwake Kariakoo.Peter alikuwa ni mtu wake wa karibu Saimon,tokea kipndi chao,walichokuwa wakisoma shule ya msingi.Peter alikuwa hodari sana shuleni,katika micezo ya maigizo,kwa hivi sasa,amekuwa akijishughulisha na kutunga nyimbo za bongo fleva.Peter ana watoto wawili wakike.mmoja anaitwa Anna,mwenye miaka 19,mwengine ni Esther mwenye miaka 21.Saimon alikwenda bafuni,kwa ajili ya kujimwagia maji,baada ya kujimwagia maji,akaenda kujipunzisha chumbani kwake.Ilikuwa ni majira ya saa kumi jioni,wakati Saimon alipokwenda kujipunzisha kitandani.Jonas alikuwa ni msichana aliyevutwa sana na Saimon,kwa wakati huo alikuwa yupo nyumbani kwao,ila mawazo yote,yalikuwa ni kwa Saimon.Jonas akajitayarisha kwa kuoga,na kujiandaa kwenda kumwona Saimon nyumbani kwao.(nini kitatokea?tutaendelea...)

No comments: