Translate

Saturday, April 21, 2012

PENZI LA MASHAKA (SEHEMU YA KUMI NA NNE)

Katika sehemu iliyopita tumeona saimon na jonas wakiwa pamoja usiku mzima,kisha saimon alikwenda mjini asubuhi na mapema,baada ya kufika mjini akakutana na Peter,wakapata muda wa kuongea na kuagana,kisha Saimon akaelekea Bamaga,alipofika akampigia simu Anita,ili waweze kukutana na kupanga mikakati ya kazi .sasa endelea..) Kama tunavyoelewa binadam huwa anabadilika kadri mazingira yanavyobadil
ika,kama ulikuwa makini mwanzo wa hadithi hii,utaona jonas na Saimon ,walikuwa wapenzi tokea mwanzo wa hadithi,kabla ya Saimon hajaenda uk ,kusoma.Lakini Saimon yule wa mwanzo ,siye Saimon wa leo,Amekuwa anabadilika kadri siku zinavyoenda mbele,Ukiangalia kwa undani kabisa,utaona Jonas ni msichana mvumilivu na mwenye upendo wa dhati kwa Saimon,hivyo inamfanya Saimon kuwa mzito katika maamuzi yake,ya kumchagua mpenzi mmoja kati ya Jonas na Anita.Lakini ukifuatilia kwa makini utaona Saimon yupo karibu na Anita kwa sababu ya tamaa ya mali,na si tamaa ya mapenzi.Hii ndio hali halisi ya maisha ya sasa,na ndio imenivuta kwa undani zaidi kuandika hadithi hii,Lengu langu haswa ni kuwakumbusha wote walio katika jamii,kuwa na msimamo na wapenzi wao,hata kama hawana kitu,kwa kufanya hivyo,mtaweza kuwa na mapenzi ya dhati na yenye furaha.Saimon akampigia simu Anita ,wakaagana kukutana bamaga.Waliweza kupanga mambo yao ya kazi,baada ya hapo,Anita akampatia Saimon pesa ya matumizi.Wakaagana na kila mmoja akarejea nyumbani kwake.Saimon alipofika sinza akakutana na Jonas,wakasalimiana kisha wakaenda chumbani kujipunzisha,walipokuwa chumbani,Jonas akamuliza Saimon,vipi leo,mbona umechelewa?Saimon akamjibu,nilikuwa na kazi nyingi,ndio maana nimechelewa.(itaendelea....)

No comments: