Translate

Saturday, April 21, 2012

PENZI LA MASHAKA(SEHEMU YA KUMI NA TANO)

Katika sehemu iliyopita tumejaribu kuwaeleza mwenendo mzima wa taswira ya hadithi hii,na tuliangalia pia ,Saimon na Anita ,walipokutana na kisha baada ya maongezi,wakaagana,kila mmoja kurejea nyumbani kwake.(sasa endelea...) Saimon na Jonas ,walikuwa kwenye maongezi chumbani,Jonas alikuwa ni msichana mwenye huruma na mpole.Jonas ni msichana mvumilivu na mwenye maadili mema kwa kila mtu.Saimon alikuwa na pesa nyingi mfukoni,akachukuwa pesa zake na kumpatia Jonas.Baada ya muda kidogo Anita akampigia simu Saimon,kwa wakati huo,Saimon alikuwa amekumbatiana na Jonas kitandani.Jonas akapokea simu ya Saimon,Anita kama kawaida yake ,akamsalimia Saimon,Habari yako Saimon?Jonas akamuliza nani wewe?Anita akamjibu ,kwani wewe ni nani?Jonas akamwambia Anita,unajuwa wewe msichana mkorofi sana,umepiga kwenye simu ya bwana wangu,halafu nakuliza nani wewe,unashindwa kunijibu,badala yake ,unaniuliza mimi nani?Kwa wakati huo,Saimon alikuwa kimya akisikiliza mazungumzo kati ya wapenzi wake wawili.Saimon hakuweza kuongea lolote mpaka ,maongezi yalipokwisha.Jonas akaweka simu ya Saimon mezani ,na akarudi kitandani alipokuwa Saimon.baada ya muda sio mrefu,usingizi ukawachukuwa na wakjikuta wamelala usingizi mzito. Asubuhi na mapema,Saimon akajiandaa kuelekea bamaga,ili aweze kuwasiliana na Anita,Saimon akatoka nyumbani kwake,wakati akiwa kituoni kuelekea bamaga,Anita akampigia simu Saimon,Baada ya kusalimiana ,Anita akamuliza Saimon,mbona unawapa simu yako,hao wanawake zako?Saimon akamjibu Anita ,samahani sana,jana kulikuwa na dharura kidogo,(itaendelea....)

No comments: