Translate

Sunday, April 1, 2012

PENZI LA MASHAKA ( SEHEMU YA KWANZA)

Katika penzi la mashaka ,tunaangalia pale,Saimon alipokuwa anatoka masomoni uingereza,akiwa amechukuwa shahada ya uchumi,katika chuo kikuu cha OXFORD ya UK.Akiwa katika Airport ya Mwalimu nyerere,Saimon,alipokelewa na rafiki yake,Jonas,pamoja na mama yake Frida.Wote walipakia kwenye gari na kuelekea Sinza ,nyumbani kwa mama yake Saimon.Walipokuwa nyumbani Sinza,Saimon alitembelewa na marafiki zake

mbalimbali,wakiwemo marafiki zake,waliosoma wote pale,shule ya sekondari ya Benjamini Mkapa.Siku hiyo ilikuwa,ni siku ya furaha kwa Saimoni,pamoja na marafiki zake,Baada ya chakula cha mchana,Saimoni alijipunzisha chumbani,kutokana na uchovu wa safari.Ilipofika majira ya saa 11 jioni,Saimon aliamka na kuenda kujimwagia maji,Baada ya hapo,akapata muda wa kula chakula cha jioni.Baada ya chakula,wakaa na ndugu zake sebuleni,na kuanza kuongea,habari za safari,pamoja na masomo,pale uingereza,Saimon alikuwa ni mtu mwenye furaha sana ,katika siku ile,kwa sababu ilikuwa ,ni siku ya kwanza kutua akitokea uingereza,alikuwa amekaa huko kwa muda wa miaka minne,alikuwa ni mtu mwenye furaha sana,kukutana na marafiki zake na familia kwa ujumla. ( itaendelea.....)

No comments: