Translate

Thursday, April 5, 2012

PENZI LA MASHAKA (SEHEMU YA NANE)

Katika sehemu iliyopita tumeona Saimon akirudi nyumbani na kukutana na Jonas,akimsubiri,Saimon na Jonas ,baada ya kusalimiana na kuelekea chumbani ,kwa ajili ya kulala.Majira ya saa 5 usiku,Anita akampigia simu,Saimon,Lakini ilikuwa ni vigumu kw saimon kupokea simu.Saimon akachukuwa taulo,na kuelekea bafuni.hapo ndipo Jonas,akamfuata Saimon nyuma,bila kuelewa.Saimon na Anita,wakati wakiwa kwenye mazungumzo,Jonas alikuwa akiwasikiliza.(Nini kitatokea?sasa endelea...)Jonas
akaendelea kusikiliza mazungumzo,mpaka walipomaliza maongezi yao,Jonas akakimbia chumbani,alipofika chumbani,akajitupa kitandani na kuanza kukoroma,kama mtu ,aliyekuwa amelala muda mrefu uliyopita.Saimon alipomaliza maongezi bafuni,akajimwagia maji,na kurudi chumbani.Alipofika chumbani,akamkuta Jonas akiwa hoi,amelala.Saimon akajisemea moyoni,nina kazi ngumu ya kuchagua mpenzi bora kwangu.Saimon akajitupa kitandani,na kuanza kulala.Ilipofika asubuhi,majira ya saa moja asubuhi,Saimon aliamka,na kuanza kujiandaa kwa ajiki ya kwenda kazini.Saimon akamwambia Jonas,usiwe na wasiwasi mpenzi,naelekea kazini,lakini ngoja nikupe pesa ya matumizi.Saimon akatoa shilingi laki moja,na kumpatia Jonas.(nini kitatokea?tutaendele,baada ya mfupi.

No comments: