Translate

Monday, April 2, 2012

PENZI LA MASHAKA(SEHEMU YA TANO)

Katika sehemu iliyopita,tumeona Anita na Saimon,wakiwa Bamaga,baada ya kukutana,na kuongea kwa kifupi(,sasa endelea...) Anita akamwambia Saimon,napenda tuwe wote siku ya leo,kwenye maeneo ya mbezi beach,Saimon akamjibu mmhhh,,,sasa vipi kuhusu kazi itakuwaje?Anita akamjibu,wasiwasi wako wewe nini?Saimon akamjibu Anita,sina wasiwasi,ila nategemea hiyo kazi,ndio itakuwa mkombozi wangu.Anita akacheka sana,kisha akamwambia Saimon,mimi ndio meneja wako,nitakupa utakachokitaka.Saimon akamwambia Anita,unajuwa mimi nina familia,na isitoshe nyumbani sisi ni masikini sana,siwezi nikakuomba kila kitu,inaweza kuwa ni tatizo kwangu.Anita akamwambia Saimon,twende mbezi beach,nitakupatia pesa,ukatatuwe matatizo ya nyumbani kwenu.Saimon kwa shingo upande,akakubali,akamwambia Anita,sawa mimi naona bora twende.
SAIMON NA MPENZI WAKE ANITA
Saimon na Anita,wakaondoka pamoja na kuelekea mbezi beach.wakiwa mbezi beach,waliagiza vinywaji na nyama ya kuchoma.wakiwa wanakula na kunywa,Saimon alikuwa anatabasam,Anita akamuuliza saimon,mbona umefurahi sana mpenzi wangu?Nimefurahi sana,kwa sababu nakupenda sana,ila khofu yangu mimi,sikutegemea kama ungenikubalia penzi lako. Anita akamjibu Saimon,mimi nakupenda sana,na sikutegemea kama ungelikubali penzi langu,lakini umenikubalia,usiwe na wasiwasi,nitakusaidia kwa matatizo yako,na nina imani,utafurahia penzi langu,nakupenda kuliko hata asali.

No comments: