Translate

Monday, April 2, 2012

PENZI LA MASHAKA(SEHEMU YA NNE)

Katika sehemu iliyopita tumeona Saimon,wakiwa wamejipunzisha kunduchi.Majira ya saa 4 usiku,wakaondoka na kurudi nyumbani Sinza.Baada ya kufika nyumbani,wakaagana na Jonas,akarudi nyumbani kwake,Saimon ,aliamka mapema na kuelekea kwenye kazi,katika kampuni ya Baba yake Anita.Saimon alipanda daladala mpaka Bamaga,kisha akampigia simu Anita.(Sasa endelea....) Anita akawasha gari moto na kuelekea Bamaga,Alipofika pale ,akamkuta Saimon amekaa nje,ana msubiri .Anita akasogeza gari lake mpaka pale ,walipokuwa amekaa Saimon,Akashuka kwenye gari,na kumkumbatia Saimon.
Anita na Saimon,wakakaa chini na kuanza kuongea kuhusu mipango ya kazi.Anita akamwambia Saimon,kuhusu mipango ya kazi,usiwe na wasiwasi,nimemwambia Baba,khusu wewe,na amekubali ,ukafanye kazi kwenye kiwanda chake cha kutengeneza software za catoon,ukiwa kama meneja msaidizi.Mimi ndio meneja.Saimon akafurahi sana kusikia hivyo,Anita akamwambia Saimon,unajuwa mimi,nakupenda sana,ndio maana ,nimefanya mipango yote,nategemea wewe ndio uwe wangu mpenzi,Kabla ya yote ,nakupa zawadi nzuri ya uwa,kuashiria kwamba,sina mwengine zaidi yako.
Simon alifurahi sana,kwa zawadi ya uwa la rosi,kuashiria alama ya upendo,kutoka kwa Anita,(nini kitaendelea?Tukutane tena baada ya muda mfupi.

No comments: