Translate

Monday, April 2, 2012

PENZI LA MASHAKA(SEHEMU YA TATU)

Katika sehemu ya pili,tumeona Saimoni,na Jonas wakiwa wamejipunzisha katika ufukwe wa Bahari,maeneo ya Kunduchi Beach,wakiwa ni watu wenye furaha,walifurahia kuwa pamoja siku ya kwanza kukutana,tokea Saimon,arudi masomoni uingereza,nini (kitaendelea---?) Ilikuwa ni majira ya saa 4 usiku,Saimon na Jonas,walikodisha gari ndogo,na kurejea nyumbani sinza.Walipofika sinza,Saimon alikuwa amechoka sana,akupoteza muda,akaenda kujipunzisha ,baada ya kuagana na jonas.Saimoni na jonas walikuwa ni majirani wa karibu sana,kuna tofauti ya nyumba tano.Asubuhi na mapema,Saimon aliamka na kujiandaa kwenda kuripoti kwenye kazi,Wakati akiwa masomoni uingereza,Saimoni alikuwa akifanya mpango wa kazi,kwa kupitia kwenye mtandao wa ZOOM.Saimoni aliweza kupata kazi,kwenye kampuni ya Baba yake Anita,ambaye walikwa wote masomoni uingereza na Anita.Saimon alikuwa amekwisha anzisha uhusiano na Anita ,wakati wakiwa masomoni uingereza.Kitu ambacho,Jonas kama atakigunduwa,anaweza,sumu na kujiuwa,kwa jinsi anavyompenda Saimon,inasikitisha kwa mwanaume kama Saimon,kuwa na tabia mbaya ,ya kuwa changanya wanawake wawili,kwa tamaa ya kitu kutoka kwa Anita.Saimon ,alipanda daladala,mpaka pale Bamaga,alipofika pale,akampigia simu Anita,ili aweze kuja mchukuwa.Baada ya kumpigia simu,Anita akawasili pale Bamaga,na kuja kumchukuwa Saimon.(
nini kitaendelea?baada ya muda kidogo,tutaendelea)

No comments: